![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
![]() |
|
| Portal | Liberation Forum | Store | Arcade | Search YouTube | ABIBItube Media | Site Map | Photo Gallery | Abibifiles | Bookmark Us! | Member Classroom |
|
|||||||
| Register | VBay [0] | Invite Afrikans | Stats | All Albums | Blogs | FAQ | Donate | Members | Calendar | Search | Today's Posts | Mark Forums Read |
| Notices |
| KiSwahili Language Resources Mkusanyiko wa Lugha ya Kiswahili |
|
|
http://www.abibitumikasa.com/forums/![]() |
|
![]() |
|
|
LinkBack | Thread Tools | Display Modes |
|
||||||||||||
|
Swahili Poems
Kitandawili Natowa Date: July 1, 2000 Author: Hashil S. Hashil, Denmark. 1. Natowa kitandawili / mwenye jawabu kutowa Wako watu sura mbili / majaraha yasopowa Kuchupa kwao kuwili / nyoyo zao zaunguwa Watakayo ni muhali / milele hayatokuwa. 2. Akili zao ni ghali / kutu zinawasumbuwa Wapigana na makali / mwenye fani hupekuwa Warejea ya awali / hawavuki zao puwa Wala hawana muhali / wamegeuka viluwa. 3. Wanapeta pili pili / ungó wao chandaruwa Upungufu wa akili / ukweli kuutambuwa Wasemavyo waawali / wengine wajisumbuwa Hatari yawakabili / kuviwasha vilopowa. 4. Mkahawa sihoteli / kushindana kutambuwa Dibeti zisoukweli / mtuno wakitumbuwa Kisu kutiwa makali / mwerevu anang´amuwa Ukweli muukubali / mwiko mwenziwe upawa. Kitandawili (Jibu) Date: July 1, 2000 Author: Hassan O. Ali, Ottawa, Canada. 1. Watu wenye sura mbili, unao wasimulia Si watu ni makubeli, wako tayari kuua Tukae nao kwa mbali, roho wasije zitoa Watu wasio murua, ni maadui wa kweli. 2. Wasifu wao tumbili, kila mti wachupia Vipando vyetu halali, haweshi kuvivamia Tena wafanya kejeli, majumbani waingia Watu wasio murua, ni maadui wa kweli. 3. Hawajali hawabali, wendekeza ya dunia Nyoyo zao za jabali, imani 'mewapotea Wanajikumbizia mali, nundu zao za ngamia Watu wasio murua, ni maadui wa kweli. 4. Asiyemcha Jalali, Muumba wetu Jalia Hafai hastahili, kuwaongoza raia Isiwe mara ya pili, fursa kumuachia Watu wasio murua, ni maadui wa kweli. 5. Beti tano ni kamili, kuongeza sina nia Kwa chako kitendawili, jibu nimekutolea Nambie ewe Hashili, kama nimekipatia Watu wasio murua, ni maadui wa kweli. Pakacha Pakachuka Date: May 24, 2002 Author: Hassan O. Ali, Ottawa, Canada. 1. Pakacha waniweka, roho juu Pakacha kila mwaka, hata huu! Pakacha wanitaka, niwe zuu? Pakacha pakachuka, chini puu! 2. Pakacha nadhikika, dhiki kuu! Pakacha ninanuka, na kupuu Pakacha wanicheka, sana tuu! Pakacha pakachuka, chini puu! 3. Pakacha umeruka, kichuguu Pakacha hujavuka, lima kuu Pakacha 'tachauka, chau chau Pakacha pakachuka, chini puu! 4. Pakacha sina shaka, si kifuu Pakacha asotaka, la mkuu Pakacha huvunjika, lake guu Pakacha pakachuka, chini puu! Pakacha Pakachuka ... (jibu) Date: May 24, 2002 Author: Bakari A. Ali, Reading, U.K. 1. Tungo ni safi nzuri, ahsantuu Utunzi huna dosari, wewe juu Waenda njema safari, ya majuu Hassani wewe hodari, ni mkuu 2. Beti zanukia wazi, karafuu Twafurahia ujuzi, ulio juu Furaha kubwa azizi, sikukuu Mkono wenye pongezi, shika huu Pakacha Pakachuka ... (jibu) Date: May 24, 2002 Author: Hashil S. Hashil, Denmark. 1. Pakacha parachuka, wajikuta chini juu Pakacha lakucheka, mzegazeka nafuu Pakacha kusarifika, zambarau sio fuu Pakacha towa talaka, ndio siri ya kifuu 2. Pakacha ni kichaka, cha mbuni vitu kuviacha wazi Pakacha mashaka, wengi wauza mbaazi Pakacha kushilanga muafaka, shabaha kupanda ngazi Pakacha kuliamini ni shaka, lageuka utelezi 3. Pakacha nakunasihi, fujo zako kuziacha Pakacha huzimi wala huwashi, wajijua umechacha Pakacha kipimo chako ni pishi,wengine watoto pacha Pakacha ubani wako mafushi, mara nyengine mchicha 4. Pakacha kujihashuwa uwache, mara hii utadunda Pakacha makarara kwako cheche, mnyama wako ni punda pakacha gari lako ni mkweche, wapakia vilovunda Pakacha miye si cheche, ni sungura kwenye sanda. Pakacha Pakachuka ... (jibu) Date: May 25, 2002 Author: Ally bin Aboubakar, London, U.K. 1. Wallahi nafurahika, ushairi kuushika, Malumbano kuyateka, na nyoyo kuburudika, Ila Pakacha nateta, jawabu hatujalipata, Pakacha hili nlipi, la Canada au Pemba? 2. Dr.nakukumbusha,pakacha la kwenu Pemba, Muhogo na wake pweza,jioni utajitweka, Masheli ya kupwaza,si haba utajitwika, Pakacha hili nlipi,mbona hwelitaja? 3. Karafuu hichumia, na mpeta kuokotea, Leo mbona mwalinunia, pakacha hili la kujivunia, Wallahi najivunia, mipesa nejichumia, Dr.Hassan hebu nambia, kabla sijakufokea, 4. Komputa hutaitia, ndani ya pakacha nakwambia, Ila ndio tweanzia, karafuu na kijio kutafutia, Hebu leo twambie, huko canada lipo hilo Pakacha Au nlile la aslia , Pemba na Unguja lanukia? N'na Paka Guniani Date: October 25, 2000 Author: Hassan O. Ali 1. Sitathubutu kusema, nimeshakula yamini Mchota maji kisima, hata iwe muadhini Hatanitoa kalima, wala hatanizaini N'na paka guniani, sitathubutu kusema 2. Paka huyu kisirani, si paka ni ngawa-nyumba Avuua kaangoni, mara akinusa vumba Jeleko la kizamani, alitipa kama pamba N'na paka guniani, sitathubutu kusema 3. Si paka ni subiani, jini amepigwa chapa Usipokaa makini, mara hukwendesha kapa Ndio hasema sineni, kanishinda namtupa N'na paka guniani, sitathubutu kusema 4. Sitasema akarudi, akazidi kunitimba Nimeifanya juhudi, mwituni nenda msumba Hutendwa lisilo budi, mdomo ninaufumba N'na paka guniani, sitathubutu kusema Heko Kwa Bwana Hassani ... (jibu) Date: October 25, 2000 Author: Ahmed Rashid 1. Japo paka subiani, shetani wa ujinini, Sasa yuko hatarini, simtoe guniani, Enenda naye porini, umfukie shimoni, Heko kwa Bwana Hassani, kalitupe paka shume. 2. Kalitupe paka shume, likatoweke mwituni, Litupe lisisimame, limetuchosha nyoyoni, Uhakika tuuseme, ni paka shume ja nyani, Heko kwa Bwana Hassani, kalitupe paka shume. 3. Paka hili jizi sana, masinzi tele usoni, Mbinuze ni nyingi sana, kuiba nyama jikoni. Hata Hassani kinena, shume harudi nyumbani, Sema siogope shume, shume harudi nyumbani. 4. Kusema usiogope, yanene yote wavuni, Na changa moto tukupe, uyatoe ya moyoni, Kwa pamoja tulitupe, shume lilo guniani, Heko kwa Bwana Hassani, kalitupe paka shume.
__________________
"Isn't it sad how some people's grip on their lives is so precarious that they'll embrace any preposterous delusion rather than face an occasional bleak truth?" |
![]() |
| Bookmarks |
| Tags |
| poems, swahili |
| Thread Tools | |
| Display Modes | |
|
|
|
These are the 70 most-searched-for thread tags
Search Tag Cloud
|
| (twi) 7 or 8 9th 2008 abibitumi abujamal africa afrikan akan ancient applications baby baruti begins bible black camps class cnn concentration court cultural death egyptians family geronimo ghana ghanafest hebrew? inside introduce journey june kamau kambon kasa languages launch learn liberation links main messengers mothers mwalimu nations network nigerian okomfo online origin post race rashidi runoko sankɔfa science seneweb session slideshow standing summer summit t'shango trouble twi week wolof words yoruba |