Semi za Kiswahili (swahili sayings)
Semi ni vifungu vya maneno yenye maana fiche - Words that have hidden meanings.
Hi ni baadhi ya semi chache nime kunited snakesnya
NB: KEY
m.y. - Maana yake (its meaning)
mat. - Matumizi (how to use)
1. Ambukia patupu
m.y. - Kosa kabisa
mat. - Aliyekuwa akitafuta kitu kwa bidii sana na akakikosa anaweza
kujisikitikia kwa kusema: Nimejitahidi juu chini lakini nimeambukia
patupu.
2. Ajabu ya shingo kukataa kulia mto
m.y. - kataa kitu ulicho na haja kubwa nacho
mat. - Usemi huu huambiwa mtu aliye na haja na kitu lakini ajifanya hana
haja nacho. Basi aweza kuambiwa: Vipi bwana? Hiyo ndio ajabu ya shingo kukataa kulalia mto
3. Amejifunga kwa ulimi wake
m.y. - Amesema maneno ambayo yanathibitisha hatia yake.
mat. - Mshtakiwa aropokaropokaye kortini anaweza kuonywa na wakili
wake kwa kuambiwa: Utajifunga kwa ulimi wako iwapo
hutazungumza kwa hadhari
4. Amekwenda mrisi
m.y. - Hajafanikiwa katika aliyotaka
mat. - Usemi huu waweza kuutimia hivi: Alitaka kuwa mbunge lakini mpaka sasa ameenda mrisi..
5. Ametumbukia kisimani
m.y. - Ameingia katika shida ambazo ni vigumu kujitoa