Sponsored Community Message Browse Free. Go deeper with Full Access. Free visitors can browse public knowledge. Full Access unlocks participation, member areas, and an ad-free experience.

Semi za Kiswahili (swahili sayings)-gctid30426

Started by KaNisa, Aug 13, 2008, 05:42 PM

Previous topic - Next topic
Semi za Kiswahili (swahili sayings)
 Semi ni vifungu vya maneno yenye maana fiche - Words that have hidden meanings.
 
 Hi ni baadhi ya semi chache nime kunited snakesnya
 
 NB: KEY
 
 m.y. - Maana yake (its meaning)
 
 mat. - Matumizi (how to use)

1. Ambukia patupu
 m.y. - Kosa kabisa
 mat. - Aliyekuwa akitafuta kitu kwa bidii sana na akakikosa anaweza
 kujisikitikia kwa kusema: Nimejitahidi juu chini lakini nimeambukia
 patupu.
 
 2. Ajabu ya shingo kukataa kulia mto
 m.y. - kataa kitu ulicho na haja kubwa nacho
 mat. - Usemi huu huambiwa mtu aliye na haja na kitu lakini ajifanya hana
 haja nacho. Basi aweza kuambiwa: Vipi bwana? Hiyo ndio ajabu ya shingo kukataa kulalia mto
 
 3. Amejifunga kwa ulimi wake
 m.y. - Amesema maneno ambayo yanathibitisha hatia yake.
 mat. - Mshtakiwa aropokaropokaye kortini anaweza kuonywa na wakili
 wake kwa kuambiwa: Utajifunga kwa ulimi wako iwapo
 hutazungumza kwa hadhari
 
 4. Amekwenda mrisi
 m.y. - Hajafanikiwa katika aliyotaka
 mat. - Usemi huu waweza kuutimia hivi: Alitaka kuwa mbunge lakini mpaka sasa ameenda mrisi..

5. Ametumbukia kisimani
 m.y. - Ameingia katika shida ambazo ni vigumu kujitoa
"Isn't it sad how some people's grip on their lives is so precarious that they'll embrace any preposterous delusion rather than face an occasional bleak truth?"